Tuesday 29 August 2017

MUUGUZI ADAIWA KUHUSIKA KATIKA VIFO VYA WATU 84 UJERUMANI………….

Muuguzi mmoja anayetumikia kifungo cha maisha jela kwa kuwauwa wagonjwa wawili kaskazini mwa Ujerumani, sasa anashukiwa kuhusika na visa 84 vya mauaji.

Hayo yamesemwa na maafisa wa polisi nchini Ujerumani.
Muuguzi huyo mwenye umri wa miaka 40, ametajwa kwa jina Niels H, chini ya sheria za kuripoti habari nchini Ujerumani, alihukumiwa kwa kosa la kujaribu kuuwa mnamo mwaka 2006 na kosa la mauwaji mwaka 2015.
Wahasiriwa wake walidungwa dawa yenye sumu, katika kitengo cha matibabu alikokuwa akifanyia kazi.
Jamaa za wagonjwa waliofariki kwenye zahanati alikokuwa akifanya kazi, wameomba polisi kuendeleza uchunguzi zaidi.
Tume maalum ilibuniwa mwaka 2014 kuchunguza ukubwa wa uhalifu huo, ambao unaweza kumfanya kuwa muuwaji mkubwa zaidi nchini Ujerumani baada ya mauwaji yaliyotokea kulipomalizika vita kuu vya kwanza na vya pili vya Dunia, pamoja na ile ya enzi ya utawala wa Nazi.
Matibabu aliyokuwa akiwapa wagonjwa, yalisababisha matatizo makubwa ya kuzima kwa moyo au kushindwa kufanya kazi kwa mishipa ya damu na matatizo ya kupumua hatua iliyomfanya mgonjwa kuanguka ghafla na kuzimia.
Baada ya mgonjwa kuonekana kama amefariki, anawapa dawa nyingine ya kuwarejeshea uhai.
Majaji wanasema kuwa, alichochewa na hamu ya kupata umaarufu na sifa kwa watu, kwa kuwarejeshea tena uhai wagonjwa aliokuwa amewapa dawa hiyo ya sumu.
Wakati wa kesi iliyofanyika mwaka 2015, alikiri kuwapa zaidi ya wagonjwa 90 dawa hiyo.
Polisi wanasema kuwa kasoro inarudi nyuma hadi mwaka 2,000 katika kliniki moja mjini Oldenburg.
Wanasema kuwa wafanyikazi walifanya mkutano mwaka 2001 kujadili viwango vya kushangaza vya vifo na na matendo ya kujaribu kufufua watu, lakini hawakuripoti visa hivyo na badala yake Niels H alihamishiwa hadi zahanati nyingine iliyoko Delmenhorst.
Tume maalum ya polisi ilibuniwa mnamo mwaka 2014 ili kuchunguza kesi hiyo.
Ilichunguza mamia ya rekodi ya kimatibabu na kufukua jumla ya maiti 134, ili kufanyia majaribio chembechembe ya dawa iliyotumika.
Uchunguzi huo aidha ulitatizwa pakubwa kwani baadhi ya maiti ya wahasiriwa ilichomwa baada ya kufa.
"Matokeo haya aidha yanaendelea kutatiza uhalisia wa fikra za watu," amesema mkuu wa polisi Oldenburg, Johann Kuhme. "sio rahidi kusema ni watu wangapi waliuwawa."
Bwa Kuhme ameonya kuwa huenda idadi ya waliuwawa ikaongezeka. Kuna uwezekano kuwa kesi mpya itawasilishwa mwanzo wa mwaka ujao wa 2018, amesema.


0 comments:

Post a Comment