Raia
wa Nigeria Oshi Agabi amezindua kompyuta zinazotumia neva za panya katika
kongamano la kiteknolojia la TEDGlobal linaloendelea nchini Tanzania.
Mfumo huo umefunzwa kutambua
harufu ya vilipuzi na unaweza kutumiwa katika kuimarisha usalama katika viwanja
vya ndege, alisema.
Vilevile kifaa hicho kilicho na
ukubwa wa modem na kupewa jina Koniku Kore kinaweza kuwa ubongo wa roboti za
siku za usoni.
Kampuni kubwa za kiteknolojia,
ikiwemo Google hadi Micrososft ziko katika harakti ya kutengeza roboti
inayoweza kuwa na akili ya mwanadamu.
Huku Kompyuta zikiwa bora
kushinda mwanadamu katika kutatua hesabu ngumu, kuna majukumu mengi ambayo
yanaweza kufanywa na ubongo wa mwanadamu ikiwemo kuifunza kompyuta kutambua
harufu.
Bwana Agabi analenga kubadili
baiolojia ya uhandisi ambayo tayari imetimiza uvumbuzi huo.''Biolojia ni Teknolojia''.
Kazi yetu kuu ni kujaribu kuiga
ubongo.
Alizindua kifaa hicho cha koniku
yapata mwaka mmoja uliopita na amefanikiwa kuchangisha dola milioni moja kama
ufadhili na anasema kuwa kifaa hicho kimempatia dola milioni 10 katika mikataba
na kampuni za usalama.
Koniku Kore ni kifaa
kilichotengezwa kwa kutumia neva na silicon ambacho kina sensa ambazo zinaweza
kutambua harufu.
Unaweza kuzipa neva hizo maelezo
ya ni unachotaka zifanye ambapo upande wetu tunaziambia kutoa seli zinazoweza
kutambua harufu.
0 comments:
Post a Comment