Mtu mmoja
ameshtakiwa na maafisa wa polisi nchini Australia kwa wizi, baada ya kuvunja na
kuingia katika nyumba moja kabla ya kunywa shampeni na kulala kitandani.
Polisi wanasema jamaa huyo wa miaka 36 alivunja na kuingia
nyumbani humo mjini Esperence, magharibi mwa Australia siku ya Ijumaa.
Alilewa baada ya kunywa kinywaji hicho, kulingana na sajenti
Richard Moore kutoka polisi ya Esperence.
Mwenye nyumba hiyo alirudi nyumbani na kumpata mwizi huyo
amelala kitandani mwake.
Ndipo alipotoka nje na kuwapigia simu polisi ambao waliwasili
na kumkamata mshtakiwa.
Mtu huyo
alipelekwa hospitalini baada ya kupatikana amelewa chakari alisema sajenti
Moore wa eneo hilo la Esperence.
0 comments:
Post a Comment