Wenye Virusi Vya Ukimwi (VVU)
wanaotumia dawa za kufubaza virusi (ARVs), wamethibitika kitaalamu kuwa
wakitumia dawa hizo kwa uaminifu bila kukatisha dozi, hawawezi kuwaambukiza
watu wengine kwa kujamiiana.
Isipokuwa
maambukizi yanawezekana endapo mtu huyo anayetumia dawa akijikata na damu
ikadondokea kwenye kidonda au eneo lenye mchubuko la mtu asiyekuwa na virusi.
Hata hivyo Ofisa Mkuu wa Uendeshaji
wa taasisi ya kimataifa inayojihusisha masuala ya afya ya Management and
Development for Health (MDH), Dk Nzovu Ulenga amehimiza utumiaji wa dawa hizo
kwa uaminifu, akisema dozi ikikatishwa, ndani ya siku 30 virusi vinaibuka tena
na maambukizi kwa wengine yanaendelea kama kawaida.
Dk Ulenga
alitoa taarifa hiyo jana kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ukimwi ya
Bunge, kwenye kikao cha kupokea na kujadili taarifa kuhusu utekelezaji wa
miradi mikubwa ya PEPFAR na Global Fund inayotekelezwa na asasi zisizo za
kiserikali nchini.
Dk Ulenga
alikuwa akifafanua hoja na maswali ya wajumbe wa kamati juu ya matumizi ya
ARVs.
0 comments:
Post a Comment