Chuo
Kikuu kimoja nchini Afrika Kusini kimesema kwamba kilituma kimakosa jumla ya
randi milioni 14 ambazo ni sawa na dola milioni moja za Marekani katika akaunti
ya benki ya mwanafunzi mmoja nchini humo.
Pesa
hizo zilitoka kwenye mfuko wa shirika la kufadhili wanafunzi kimasomo nchini
humo NSFAS.
Chuo
Kikuu cha Walter Sisulu, kinasema kuwa pesa hizo ziliwekwa miezi mitano
iliyopita, huku makosa hayo yakijulikana baada ya risiti ya akaunti ya mwanafunzi
huyo kuonyesha kuwa na mamilioni ya pesa baada ya kuwekwa katika mtandao wa
kijamii.
Chuo
hicho kikuu sasa kinachunguza ni kwa nini mwanafunzi huyo hakupiga ripoti ya
kuwepo kiasi kikubwa hivyo cha pesa kwenye akaunti yake.
Mwanafunzi
huyo amekanusha madai hayo.
Ripoti
ya shirika la habari la EWN inasema picha zimeonekana kwenye mitandao ya
kijamii, zikionyesha mwanafunzi huyo wa kike huyo akijisifu na kujionyesha
kwenye sherehe moja huku akijiburudisha na vitu vizuri vizuri, kama vile simu
mpya ya rununu.
Inaaminika
kwamba mwanafunzi huyo tayari ametumia randi 400,000.
Msemaji
wa Chuo hicho Kikuu Yonela Tukwayo amesema kuwa, pesa hizo ziliwekwa kwenye
akaunti hiyo kimakosa na kampuni ambayo inasimamia fedha za hazina ya kitaifa
za msaada wa karo ya wanafunzi (NSFAS) ambayo inajulikana kama Intellicard na
kwamba ni sharti mwanafunzi huyo arejeshe fedha hizo.
0 comments:
Post a Comment