Kampuni ya simu za
mkononi ya Sumsung, imezindua simu yake mpya ya Galaxy Note 8, ambayo ni ya
kisasa zaidi na yenye ushindaji zaidi katika soko.
Hatua hii inakuja baada ya kampuni hii kupata msukosuko
wa kibiashara ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu ilipotoa simu aina ya Galaxy
note 7 ambayo betri zake zilikuwa zinalipuka hivyo kulazimika kutolewa sokoni.
Kampuni hii ya Sumsung kutoka
Korea kusini, katika toleo hili jipya la simu ya Galaxy note 8 imekuja na vitu
vipya katika teknolojia ya usalama, ambapo ina uwezo kutambua muonekano wa
mmiliki wa simu, alama za vidole, mboni ya jicho na mfumo mpya wa kiusalama
ujulikanao kama Samsung Bixby ambayo inatoa sauti maalumu za maelekezo ya
kuweka ulinzi wa siri wa simu hiyo ubora mpya wa picha.
Simu hii ya Note
8,imekuja na kioo chenye upana wa nchi 6.3 kutoka kona moja na
nyingine,ongezeko la ukubwa wa nchi 0.1 ikilinganishwa toleo la S 8.
0 comments:
Post a Comment