Friday 11 March 2016

MTANZANIA ATAJWA KINARA WA USAFIRISHAJI DAWA ZA KULEVYA..!!

Serikali ya Marekani imeamua kutaifisha mali za mfanyabiashara wa dawa zilizopigwa marufuku za kulevya kutoka Tanzania Ali Khatib Haji Hassan maarufu kwa jina la Shikuba.

Wizara ya fedha nchini Marekani imemtaja raia mmoja wa Tanzania Ali Khatib Haji Hassan na mtandao wake, kama kinara wa usafirishaji wa dawa za kulevya kwa kushiriki katika usafirishaji wa kimataifa wa dawa za kulevya.
Kwa hatua hiyo marekani ilimuwekea vikwazo Hassan na jamaa wanaohusika naye kwenye harakati hizo, na kupoteza sifa ya kupata Viza ya kuingia Marekani.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Fedha ya Marekani mjini Washington hapo Jumatano ilisema kuwa, Hassan alikuwa akihusika katika usafirishaji wa shehena kubwa za dawa za kulevya kwenda mataifa ya Afrika, ulaya, Asia na Marekani.
Hassan alikamatwa na serikali ya Tanzania mwaka 2014, kwa kujaribu kuingiza kiasi cha kilogram 210 za dawa aina ya heroin mwaka 2012.

Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania bibi Virginia Blaser, amesema katika taarifa yake kuwa Marekani imefurahi kushirikiana kwa karibu na Tanzania, katika kudhibiti vitisho vinavyotokana na wafanyabiashara wa dawa za kulevya kama Hassan na mitandao ya kihalifu inayowasaidia.ra wa dawa za kulevya kama Hassan na mitandao ya kihalifu inayowasaidia

Kiwale 11 Blog imemnasa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Balozi Augustine Mahiga, na kwanza anaeleza iwapo serikali ya Tanzania inafahamu lolote kuhusiana na swala hilo.

0 comments:

Post a Comment