Wednesday 23 March 2016

DUBAI: SHISHA NI MARUFUKU KWA WAJA WAZITO…

Dubai imepiga marufuku wanawake waja wazito, kuvuta ama hata kuingia katika migahawa inayouza Shisha.

Hatua hiyo inafuatia shinikizo la kuimarisha afya ya umma na haswa afya ya mama waja wazito.
Sheria hiyo inawadia baada ya kampeini ya kuwazuia wanawake wajawazito kuingia pahala panapovutiwa sigara jarida la Gulf News limesema.
Kampeini hiyo inayoendeshwa kwa kutumia mabango na picha ya mwanamke mjamzito akiambiwa na mwanaye aliyeko tumboni kuwa ''Uamuzi wa kuvata au la ni wako sio wangu''
Mabango hayo yanaeleza kuwa watoto ambao hawajahitimu miaka 18 na wanawake wajawazito hawaruhusiwi kuvuta shisha au sigara.
Mkurugenzi wa afya ya umma wa Dubai bwana Marwan Al Mohammed,amesema kauli hiyo ni ya serikali wala sio hoja ya kujadiliwa na mtu yeyote.
Wamiliki wa vilabu vya burudani vinavyouza shisha, wamekuwa wakilalamikia kutokuwepo kwa sheria zinazoharamisha wanawake wajawazito kutoingia katika vilabu hivyo.
Mwaka wa 2014 milki hiyo ya kiarabu ilipitisha sheria kali dhidi ya uvutaji wa sigara, ambayo ilipiga marufuku matangazo ya aina yeyote ya kibiashara ya Sigara.
Vilevile sheria hiyo ilipiga marufuku uvutaji wa sigara ndani ya gari, iwapo mna mtoto mwenye chini ya umri wa miaka 12.

Aidha sasa kuna sheria inayotoa mwelekeo ya ni wapi shisha itauzwa, na itaruhusiwa kuwepo umbali gani kutoka kwenye makazi ya watu.

0 comments:

Post a Comment